ads

Shairi: Uliye Mwema Rafiki

 


Shairi: Uliye Mwema Rafiki

Nasema kwa tafsida, maneno napangilia

Kwenye moyo sina shida, nataka kuelezea

Mimi kwangu kawaida, ikiwa nimeridhia

Karibu ukaribie, chini moyo utulie

 

Karibu ukaribie, uliye mwema rafiki

Karibu ni hadithie, lipi lililokudhiki

Karibu name nijue, sihitaji halaiki

Kipenzi wewe ndo mie, moyo chini utulie

 

Kabla kuhadithia, niseme lilo moyoni

Huzuni imenitua, sijakuona machoni

Sina budi kuridhia, japo tiba siiyoni

Salamu ikikutua, kamwe usije nihini

 

Salamu zangu pokea, kutoka kwangu moyoni

Nafurahi kusikia, bado upo kivulini

Mwendo ukiufikia, mtangulize manani

Mola atakuridhia, ufurahi maishani

 

Ufupi maisha yetu, yata kinga rafiki

Rafiki alo mwenzetu, bila chembe unafiki

Ajue kilio chetu, machozi yakidiriki

Baraka za mola wetu, juu yetu zidiriki

 

Nakuomba samahani, nikate kwanza stori

Lipo jambo kiundani, kuwa nawe kama zari

Upendo uso kifani, kwa uzuri si hariri

Kwaheri naacha peni, nakupenda si utani.


Mtunzi: Mwinyi Abdallah Khatibu

              0655895599

   Email: Mwinyiabdallah2012@gmail.com

Post a Comment

0 Comments